Chaguzi za Shirika la Wikimedia/2022/Tangazo/Kipindi cha Upigaji Kura wa Jumuiya kwa Uchaguzi wa Bodi ya Wadhamini wa 2022 sasa kimefunguliwa
Outdated translations are marked like this.
Kipindi cha Upigaji Kura wa Jumuiya cha Uchaguzi wa Bodi ya Wadhamini wa 2022 sasa kimefunguliwa
Habarini nyote,
Kipindi cha Upigaji Kura wa Jumuiya kwa Uchaguzi wa 2022 wa Bodi ya Wadhamini sasa kimefunguliwa
- Jaribu Dira ya Uchaguzi, inayoonesha jinsi wagombea wanavyosimama kwenye mada 15 tofauti.
- Soma taarifa za mgombea na majibu kwa maswali ya Washirika
- Pata maelezo zaidi kuhusu ujuzi ambao Bodi inatafuta na jinsi Kamati ya Uchambuzi ilipata wagombea wenye ujuzi huo
Ikiwa uko tayari kupiga kura, unaweza kwenda kwenye ukurasa wa kupigia kura wa SecurePoll ili kupiga kura sasa. Unaweza kupiga kura kuanzia tarehe 16 Agosti hadi tarehe 30 Agosti 2022 23:59 UTC. Ili kuona kuhusu ustahiki wako wa mpiga kura, tafadhali tembelea ukurasa wa ustahiki wa mpiga kura.
Wenu,
Mkakati wa Harakati na Utawala
Ujumbe huu ulitumwa kwa niaba ya Kikosi Kazi cha Uteuzi wa Bodi na Kamati ya Uchaguzi